Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania,Hashim Lundenga akiwa pamoja na Meneja wa Kinywaji cha Redd's Original ambao ndio wadhamini wakuu wa Shindano la Redd's Miss Tanzania,Victoria Kimaro wakiwapokea Warembo wanaoshiriki shindano hilo wakati wakiwasili kwenye Hoteli ya Giraffe,Mbezi Beach jijini Dar es Salaam leo tayari kwa kuanza rasmi Kambi yao.

 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni Lino International Agency ambao ni Waandaaji wa Shindano la Miss Tanzania,Hashim Lundenga akizungumza machache wakati wa kuwakaribisha Warembo hao wa Redd's Miss Tanzania 2013/14 walioanza kambi yao rasmi leo kwenye Hoteli ya Giraffe,jijini Dar es Salaam.
 Meneja wa Kinywaji cha Redd's Original ambao ndio wadhamini wakuu wa Shindano la Redd's Miss Tanzania,Victoria Kimaro akizungumza machache wakati wa kuwakaribisha Warembo hao wa Redd's Miss Tanzania 2013/14 walioanza kambi yao rasmi leo kwenye Hoteli ya Giraffe,jijini Dar es Salaam.
Warembo wakiingia hotelini. 
Mkuu wa Itifaki kwa Kamati ya Miss Tanzania,Albert Makoye akitoa maelekezi kwa Warembo hao.