Eneo la TRA, jijini Arusha.
Mwanamke mfanyabiashara aitwaye Valieth Mathias amepigwa risasi ya mkononi leo akiwa katika Benki ya CRDB eneo la TRA, jijini Arusha baada ya kutokea mabishano kati yake na polisi wa benki hiyo.
Chanzo cha  tukio hilo kinasema kwamba Valieth Mathias alifika maeneo ya Benki ya CRDB na kupaki gari yake akitaka kuingia benki lakini akaambiwa eneo hilo halifai kupaki gari, alipaki gari na kuingia ndani alipotoka alikuta gari lake limetolewa upepo na ndipo vurugu ilianza baina yake na polisi.
Vurugu ilipokuwa kubwa mama huyo aliwaambia polisi kwamba wasimtishie bunduki hata yeye anayo na alipotaka kuitoa polisi wakampiga risasi mkononi. Mama huyo ni muuzaji maarufu wa madini jijini Arusha na baada ya tukio hilo amekimbizwa hospitali kwa matibabu.