Mkuu wa mkoa wa Mwanza,Mh. Evarist Ndikilo (aliesimama) akitoa ripoti fupi mbele

ya wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Wizara ya Nishati

na Madini juu ya miradi inayotekelezwa na Wakala wa Umeme Vijijini

walipomtembelea ofisini kwake ili kuelezea nia yao ya kufanya ziara katika

mkoa huo.


Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Wizara ya Nishati na Madini

wameanza ziara ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na

wizara hiyo kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) katika mikoa ya kanda

ya ziwa.


Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Victor Mwambalaswa,

kamati hiyo ilipata nafasi ya kupokea taarifa fupi kuhusu utekelezwaji wa

miradi hiyo iliyosomwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist

Ndikilo ambaye aliwaeleza namna sekta hiyo inavyochangia katika kuinua

vipato vya wananchi na taifa kwa ujumla. 


Akitoa taarifa kuhusu mahitaji ya umeme Mkoani humo alieleza kuwa kiasi

cha juu kinachotumiwa na mkoa huo ni megawati 46 na kuongeza kuwa ,

kiasi hicho kinaonesha mahitaji halisi na umuhimu wa nishati hiyo na

namna umeme unavyochangia ukuaji wa uchumi mkoani humo.


Akizungumza kuhusu ujenzi wa miundombinu ya umeme, alieleza

kuwa ujenzi huo umeshika kasi na kuongeza kuwa tayari tayari mradi

uliotekelezwa na Millenium Challenge Corporation (MCC) umekamilika

wakati miradi mingine inayotekelezwa na REA na Electricity Five

inaendelea ambapo takribani wilaya 9 za mkoa wa mwanza zimeguswa na

miradi hiyo.

Aidha alisema mradi wa REA phase 1 unajegwa na mkandarasi toka

Symbion umegusa wilaya ya Sengerema, Magu na Ukerewe, REA awamu

ya pili utaigusa wilaya za Magu, Misugwi, Ukerewe, Sengerema na kwimba

na kumalizia kwa mradi wa electricity five unaofadhiliwa na Benki ya

Maendeleo Afrika kuwa unagusa wilaya za Magu, Misubwi, Kwimba,

na Sengerema ambapo alisema katika mradi huo ulipwaji wa fidia kwa

wananchi watakaoathirika umeshaanza. 

‘‘Kazi ya usambazaji wa umeme Mkoani Mwanza inakwenda vizuri,

kukamilika kwa miradi hii kutasaidia vijiji vingi kuwasha umeme hivyo

kukuza pato la taifa’’ alisema Ndikilo.

Alimalizia kwa kuwataka wajumbe hao kuwafahamisha wananchi kutumia

vipato na akiba zao katika kujenga nyumba zenye ubora ili waweze

kuunganishwa na huduma ya umeme.

Vilevile Mhe Ndikilo aliwaomba wajumbe kuwaeleza wananchi

wanaowahudumia kujenga mazoea ya kuwa na mwamko wa kupokea na

kupenda maendeleo yanayopelekwa kwao na serikali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati jhiyo Mhe. Victor Mwambalaswa

akipokea taarifa hiyo alieleza kuwa nia ya serikali ni kuhakikisha kuwa idadi

ya watu waliounganishiwa umeme inapanda toka asilimia 14 hadi kufikia

asilimia 30 ifikapo 2015.