Majeshi ya AMISOM yamekuwa yakipambana na wapiganaji wa Al Shabaab na kudhibiti baadhi ya maeneo waliyokuwa wameyateka
Raia wa Kenya waliotekwa nyara na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Al Shabaab mwaka mwaka 2011 nchiniSomalia, wameokolewa na wanajeshi wa Kenya
Wakenya hao walikuwa wanafanyia kazi mashirika ya misaada ya kibinadamu .Daniel Njuguna ambaye alikuwa akifanya kazi katika shirika la Madaktari wasio na mipakaMedecins Sans Frontieres MSF na James Kiarie wa Shirika la Care International, walikaguliwa kiafya na walitarajiwa kupelekwa Nairobi.
Awali walikuwa chini ya uangalizi wa majeshi ya Kenya ambao ni sehemu ya kikosi cha Umoja wa Afrika kilichopo nchini Somalia AMISOM.
Kenya ilipeleka majeshi yake kwenda nchini Somalia mwaka 2011 kujiunga na AMISOM kufuatia matukio ya utekaji nyara yaliyokuwa yakiendeshwa na wapiganaji wa Al shabaab katika mipaka ya nchi hiyo na Somalia.
Majeshi ya AMISOM yakishirikiana majeshi yale ya serikali ya Somalia yamekuwa yakiendesha mapambano dhidi ya wapiganaji wa Al Shabaab ambao wanafadhiliwa na kundi la kigaidi la al Qaeda linaloshikilia maeneo ya kusini na katikati mwa Somalia.