Afande Sele akiweka udongo kwenye kaburi la mke wake Mama Tunda leo jioni katika makaburi ya Kolla yaliyopo Manispaa ya Morogoro.
MAMIA ya wananchi wa Mkoa wa Morogoro wakiongozwa na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania 'TAFF', Simon Mwakifwamba wameungana kumzika mke wa mwanamuziki Seleman Msindi 'Afande Sele', marehemu Asha Mohammed Shiengo (34) 'Mama Tunda' katika makaburi ya Kolla yaliyopo mkoani humo.
Mama Tunda amefariki dunia usiku wa kuamkia leo akiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro baada ya kuugua ghafla ugonjwa wa Malaria.