Majeraha ya mguuni aliyopata Suedi Waziri baada ya kushambuliwa na Madee.
Kufuatia msala huo, msanii huyo alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Kigamboni na baadaye kuwekewa dhamana na baba yake ambapo kesi yake itatajwa tena Oktoba 6, mwaka huu.
Madee anadaiwa kumteka Suedi na kwenda kumsulubu nyumbani kwake Manzese baada ya kijana aliyekuwa amepakia kwenye bodaboda yake kukwapua simu ya msanii huyo na kukimbia.
Katika kushinikiza simu yake irudishwe ndipo Madee alipomtaiti Suedi na mwisho wa siku akaishia mikononi mwa polisi kwa kufunguliwa kesi iliyosomeka: VJB/RB/625/2014 KUTEKWA KWA BINADAMU
Imeandikwa na Mayasa Mariwata, Shani Ramadhani na Rhoda Josiah.
Imeandikwa na Mayasa Mariwata, Shani Ramadhani na Rhoda Josiah.
0 Comments