Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Karume huko Pemba na kupokewa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Ndugu Mwanajuma Majid Abdalla tarehe 20.2.2015. Mama Salma alialikwa Pemba kama Mgeni Rasmi kwenye sherehe ya Maulid ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) iliyoandaliwa na Al-Madrasat Jabal- Hiraa.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na viongozi mbalimbali waliofika kumpokea wakati alipowasili kwenye Uwanja wa ndege wa Karume huko Pemba kwa ziara ya kikazi ya siku moja kisiwani humo tarehe 20.2.2015.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa rasmi kwa kuvishwa shada na wasichana wa Almadrsat Jabal-Hiraa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Shule ya Utaani huko Wete Pemba ilikofanyika sherehe ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) ambapo Mama Salma Kikwete alikuwa mgeni rasmi tarehe 20.2.2015.