Pichani ni binti yangu Sharon.
Binti yangu huyu ni mdadisi sana na ana maswali ambayo hupendelea kuniuliza pindi anapokiona kitu ambacho kwake ni kigeni kwenye fikra zake na hutaka kujifunza.Picha hii nilimpiga kipindi cha kiangazi mwaka 2011,pindi alipotumia muda mwingi kuyaangalia hayo maji yanayomwagika kwa staili ya aina yake.alikuwa akiyaangalia huku akivuta hisia ya kitu fulani..sikutaka kumuuliza lolote kwani nilijua kama kawaida yake badala ya kumuuliza ataniuliza kwani ndio utaratibu wake.
Haikuwa vile nilivyotarajia...nilipomuita na kumuomba tuendelee na safari yetu hakusita kugeuka na tukaendelea na safari yetu.Nilitarajia swali litakuja mbeleni na hivyo nikawa najipanga kumjibu swali au maswali yake atakayoniuliza kuhusu utazamaji wa maji yale.Mpaka tunafika safari yetu hakukuwa na swali lolote kuhusiana na maji yale.Nikawa najiuliza kwanini leo binti yangu hakuniuliza swali? na sio kawaida yake kukaa kimya pindi akiona kitu ambacho ni kigeni kwenye fikra zake?.Au alikuwa na jibu la kipekee ndani ya fikra zake?au alikuwa hayupo na maji yale kifikra?.hiyo ilikuwa mwaka 2011, binafsi nilijuliza na naendelea kujiuliza kwanini sikuulizwa?
Kwa mfano huu ulishawahi kujiuliza kuhusiana na mwanao? na kama hukujiuliza unasubiri nani atakuuliza? Muulize mwanao kwanini hakuulizi maswali ? kwa kufanya hivyo utakuwa na utaratibu wa kumuuliza na kumpa changamoto ya akili yake,uwezo wa kufikiri,uwezo wa kujibu,kujifunza na kujua mambo mengi ya kujibu na kupata ufumbuzi wa yeye kuwa na maswali ya kukuuliza,usisubiri kama mimi.[somo, jifunze ndugu]
Nawatakia jumapili njema.tukutane jumapili ijayo ila sitakuuliza kwanini hukujiuliza kwani hata mimi sikuulizwa..
Maganga One~ Blogger

0 Comments