Rais Obama na Castro wakiamukuana
Viongozi wa marekani na Cuba wamefanya mkutano wao wa kwanza tangu zaidi ya nusu karne iliyopita.
Rais Obama na mwenzake wa Cuba Raul Castro walikutana ana kwa ana pembezoni mwa mkutano wa nchi za Amerika nchini Panama.
Mkutano huo utatoa mwelekeo wa kuboresha uhusiano baada ya miongo kadha ya uhasama kati ya Marekani na kisiwa hicho cha utawala wa kikoministi
Rais Obama alisema kuwa angependa kuona watu wa Cuba wakiendelea kuishi kwa uhuru na kwa usalama. Naye Castro kwa upande wake alisema kuwa Cuba ilikuwa tarayi kujenga urafiki na marekni lakini akaongeza kuwa nchi hizo mbili zina tofauti nyingi na historia iliyokumbwa na utata.