Image copyrightEPA
Image captionMawaziri wa nchi za ulaya
Mawaziri wa masuala ya ndani wa nchi za ulaya wakutana mmji Paris hii leo kujadili njia za kuboresha usalama kwenye usafiri wa reli baada ya shambulizi lililotibuka wiki iliyopita kwenye treni iliyokuwa safarini kutoka Amsterdam kwenda Paris.

Ufaransa inataka kutangaza hatua kali za usalama ikiwemo vifaa vya kutambua chuma kwenye treni za kimataifa, kuweka wahudumu waliojihami na mifumo ya mawasiliano iliyoboreka kufuatilia mienendo ya wanamgambo walioshukiwa.
Image copyright
Image captionMshambuliaji raia wa Morocco
Raia wa Morocco ambaye alikuwa amejihami vikali (Ayub al-Khazani) ambaye alishindwa nguvu na abiria baada kupanda treni mjini Brussels alikuwa akifanya safari kote barani Ulaya hata baada uhispania kutoa onyo kuwa huenda mtu huyo alikuwa ni gaidi.