Image captionTatizo la chakula ni kubwa Somalia
Umoja wa Mataifa umeelezea viwago vya utapiamlo na hali ya usalama wa chakula nchini Somalia kama vilivyo vibaya.
Unasema kuwa idadi ya watu ambao wanakabiliwa na ukosefu wa chakula imeongezeka kwa karibu asilimia 20 katika muda wa miezi sita iliyopita.
Hali hiyo inatarajiwa kuwa mbaya kutokana na ukosefu wa mvua na mzozo unaoendelea.

Karibu theluthi moja na watu nchini Somalia wanahitaji msaada wa kibinadamu. Watu robo milioni wameaga dunia nchini Somalia wakati njaa ilipoikumba nchi hiyo miaka minne iliyopita.