Mbonimpa
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon ametaka uchunguzi wa kina ufanywe kwa shambulio lililofanywa dhidi ya mwanaharakati wa haki za binadamu nchini Burundi.
Pierre Claver Mbonimpa alijeruhiwa vibaya baada ya mtu aliyejihami kumpiga risasi usoni na kutoroka kwa pikipiki.
Mwanawe Mbonimpa, Amandine Nasagarare ameambia BBC kuwa babake bado amelazwa hospitalini japo hali yake sasa imeimarishwa.