Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  DK. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumzana na wadau mbilimbali wa mpira wa kikapu (NBA) juu ya Timu bora nane kutoka kila kundi zitakazofuzu kushiriki kweye ngazi ya mitoano  Oktoba 2016. Timu bora mbili kutoka kila kundi zitakutana kwenye michezo kuwania ubingwa ili kumpata Bingwa wa kwanza wa ligi ya mpira wa kikapu kwa vijana,  katika uzinduzi wa Ligi ya Mpira wa kikapu ya vijana,leo jijini Dar es Salaam


 Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizindua Ligi ya Mpira wa kikapu ya vijana (Junior NBA) jijini Dar es Salaam Jumamosi kwa ku-shoot kikapu kwa ustadi. 

 Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali baada ya kuzindua  Ligi ya Mpira wa kikapu ya vijana (Junior NBA) jijini Dar es Salaam Jumamosi   

Rais Mstaafu DKT. Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Mchezaji Mwandamizi wa (WNBA) Allison Feaster katika uzinduzi huo  jijini Dar es Salaam

Sehemu ya mashabiki wa  Mpira wa kikapu   waliofika katika uzinduzi wa Ligi ya Mpira wa kikapu ya vijana,leo jijini Dar es Salaam.

(Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii)