Blogger wa Maganga One leo alitembelea balozi za Tanzania nchini Ubelgiji kupata huduma za nyumbani akiwa nje ya nchi.Mapokezi na huduma aliyopata aliyafurahia sana na anatoa wito kwa wale wote wenye shida kuhusiana na mambo yanayohusu balozi zetu wasisite kufika ubalozini kwa huduma na ushauri.Pichani Maganga One akiwa na afisa ubalozi mama Mndolwa.

Maganga One Blogger akiwa na baadhi ya watanzania waliofika kupata huduma ubalozini,kila mmoja aliondoka akiwa na furaha kwa kuhudumiwa vile alivyotaraji.

Pichani Maganga One akitoa mkono wa shukrani kwa afisa ubalozi mama Mndolwa kwa huduma nzuri,kushoto ni aunt Begum akiwa na binti yake Chantal ambao nao walifika ubalozi kwa kupata huduma ofisini hapo.Maganga One Blog inatoa shukrani za dhati kwa mapokezi na ukarimu alioupata ubalozini hapo.