Polisi nchini Zambia wamesema watu wawili wamechomwa moto mjini Lusaka katika vurugu ya ubaguzi wa wenyeji dhidi ya wageni.
Watu Zaidi ya mia mbili na hamsini wamekamatwa baada ya maduka mengi yanayomilikiwa na wanyaruanda kuvamiwa.Uvamizi huo ulitokea baada ya wanyaruanda kushutumiwa kuua watu na kutumia viungo vyao kuvutia wateja.

o Padre Charles Chilinda ameiambia BBC kuwa kanisa lake linafanya jitihada zote ili kuweza kuwasaidia wahanga ambao wamekwenda kuomba hifadhi kanisani.
"Kitu ambacho tunaweza kuwapa ni kwamba watakuwa na usalama wa kutosha kuwa hapo,tutaenda kuwaangalia na kuwaeleza kuwa hawa sio wazambia ambao wanagombana nao.hali hii haikubaliki ,kila mtu aliyepo katika ardhi ya Zambia analindwa na katiba ya Zambia.Ni jukumu letu kudumisha Amani na tushirikiane katika kulitokomeza hili"