Haya basi , Maafisa wa usalama wa kitengo cha kumlinda rais wa Zimbabwe Robert Mugabe walilazimika kumsogelea kwa karibu mno kiongozi huyo mkongwe katika tukio lililowaudhi raia wengi waliofika katika uwanja wa kitaifa jijini Harare kwani hata wenyewe hawakuweza kumtazama ''baba wa taifa''
Yamkini kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 92 aliingia katika uwanja wa kitaifa akiwa kwenye gari rasmi la Kijeshi
Hata hivyo baada ya kukagua gwaride la jeshi maafisa hao wa usalama walipanga kikamilifu njia ya kumstiri rais Mugabe asije akakungua na kuanguka kama ilivyokuwa mwaka uliopita
Bw Mugabe alikuwa akiongoza taifa katika kuadhimisha miaka 36 ya uhuru kutoka kwa minyororo ya ukoloni.
Rais Mugabe aliwaomba radhi wafanyikazi wa serikali waliostaafu kwa kuchelewa kupata malimbikizi ya marupurupu yao
''Bila shaka malipo yenu na mishahara ya siku za usoni itawafikia kwa muda ufaao'' alisema rais Mugabe.
Taifa hilo limekumbwa na udhaifu wa sarafu yake baada ya sera ya serikali ya kuwapokonya wakoloni wazungu mashamba na kisha kuyagawanyia waafrika weusi ambao ndio wengi kukosolewa vikali na mataifa ya magharibi yakongozwa na Uingereza.
0 Comments