Rais wa Rwanda Paul Kagame ametangaza kwamba hakuna sababu hata moja itakayoifanya nchi yake kumkamata rais wa Sudan Omar al-Bashir ikiwa ataalikwa kuhudhuria kikao cha Umoja wa Afrika kitakachofanyika nchini Rwanda mwezi Julai mwaka huu.

Rais Bashir anasakwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita (ICC) kwa tuhuma za uhalifu wa kivita na mauaji katika jimbo la Darfur.
Rwanda si mwanachama wa mahakama ya ICC.
Kutoka Kigali Yves Bucyana anaarifu.