Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na waTanzania waliojumuika kumsikiliza jijini London


Kipindi cha JUKWAA LANGU hukujia kila Jumatatu kikiongozwa na Mubelwa Bandio toka Beltsville Maryland, USA, kuzungumzia mambo mbalimbali yanayoihusu Tanzania ya sasa na ile tuitakayo.

Ni Tanzania kutoka jicho la DIASPORA

Na katika kipindi cha juma hili, tulizungumza na Chris Lukosi, ambaye
alitupa muhtasari wa ziara ya Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Kassim
Majaliwa huko nchini Uingereza.

Muhtasari huo ulizua na mjadala mkali juu ya ahadi za serikali kuhusu vibali maalum kwa waTanzania waishio nje ya nchi.

Karibu