Mgombea anayepewa nafasi kubwa ya kupeperusha bendera ya Republican katika kinyanganyiro cha urais huko Marekani Donald Trump amesema muda umefika kwa nchi hiyo kutafakari kwa kina juu ya matumizi ya taarifa binafsi za watu katika harakati za kupambana na uhalifu.

Bwana Trump aliyasema hayo katika mahojiano ya moja kwa moja na kituo cha habari za CBS akijaliana juu ya mpango wa siku za usoni wa taifa hilo,kufuatia mauaji yanayokithiri nchini humo, na hasa la hivi karibuni katika klabu moja ya usiku mjini Orlando yaliyojiri wiki iliyopita.
Ameongeza kusema kwamba nchi zingine zimetumia mbinu tata za rangi ya mtu , dini, utaifa au ukabila kama mbinu ya kutambua nani anaweza kufanya uhalifu.