Zaidi ya wanafunzi 200 nchini Burundi wamefukuzwa kutoka taasisi za elimu baada ya picha za rais Pierre Nkurunziza kuharibiwa.
Maafisa walisema kuwa wanafunzi katika eneo la Gahinga mashariki mwa nchi, waliadhibiwa kwa kukataa kumfichua yule aliyetekeleza kitendo hicho.

Mapema mwezi huu, watoto wa shule 6 ni kati ya watu waliokamatwa kwa madai kuwa waliharibu picha za rais zilizo katika vitabu vya shule vya kusoma.
Burundi imekumbwa na ghasia tangu bwana Nkurunziza kuwania na kushinda urais kwa muhula wa tatu mwaka uliopita.