Koffi-Olomide
Mwanamuziki nguli kutoka nchini Congo Koffi Olomide.
HUKUMU ya mwanamuziki nguli kutoka nchini Congo Koffi Olomide itatolewa leo jumatano katika mahakama moja mjini Kinshasa.
Hukumu hiyo itatolewa baada ya kukamatwa na polisi jana asubuhi akiwa kwenye makazi yake mjini Kinshasa, Congo na kisha kulala mahabusu katika kituo cha polisi alikofanyiwa mahojiano.
Uamuzi wa kukamatwa na kisha kuwekwa kizuizini ulitolewa na mwendesha mashtaka mkuu wa mji wa Kinshasa.