Mjadala mkali umeendelea nchini Tanzania Kufuatia waziri wa afya wa nchi hiyo kupiga marufuku utumiaji na usambazaji wa vilainishi vinavyotumiwa na wapenzi wa jinsia moja.
Waziri huyo wa Afya Ummy Mwalimu hapo juzi alitanganza kupiga marufuku vilainishi hivyo kwa madai kwamba vimekuwa vikitumiwa vibaya na wapenzi wa jinsia moja na hivyo kusababisha kuenea kwa maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Hata hivyo muda mfupi baada ya marufuku hiyo raia wa nchi hiyo walikuwa maoni tofauti.
Mjadala huu uliibuka siku chache baada ya kauli ya hiyo ya waziri wa Afya wa Tanzania Ummy Mwalimu alipozungumza na waandishi wa habari kuthibitisha kuzuiwa usambazaji wa vilainishi hivyo akidai kuwa inatumika kwa namna ambayo sio sahihi.
Wananchi wa nchi hiyo wengi wanataka suala hilo kujadiliwa kwa upana na serikali ifahamu wapi penye tatizo ili liweze kutatuliwa.
Vilainishi hivi vinavyotajwa kuwa chanzo cha maambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa kuhusishwa zaidi na watu wa mapenzi ya jinsia moja.
Hata hivyo,Wataalam wa masuala ya afya wanathibitisha kuwa yapo matumizi mengi yatokanayo na vilainishi hivi iwapo vitatumika ipasavyo.