Rais wa Brazil ambae amesimamishwa, Dilma Rousseff, amewaambia maseneta kuwa yeye ni mhanga wa njama za kisiasa, zilizopangwa na wale ambao aliwashinda katika uchaguzi mkuu miaka miwili iliyopita.
Amesema faida za kijamii za muongo mmoja uliopita zilikuwa hatarini.

Rousseff anachunguzwa na ma seneta katika hatua za mwisho za mashtaka yanayomkabili huko Brasilia.
Anatuhumia kwa kuipindisha bajeti ya nchi kuelekea uchaguzi mkuu.
Kumekuwa na maandamano yanayomuunga mkono Rousseff katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Katika mji wa Sao Paulo, polisi wametumia gesi ya machozi kuwatawanya waandamaji.apo rubo tatu ya maseneta watapiga kura dhidi yake mwishoni mwa juma, basi Rousseff ataondoka madarakani moja kwa moja.