Idadi ya watu waliofariki katika ajali ya boti iliyokuwa imebeba wahamiaji haramu wanaokadiriwa kufikia mia sita, iliyozama nje kidogo ya pwani ya Misri imeongezeka na kufikia 42.
Mamlaka nchini humo zinasema mpaka sasa watu wengine laki moja na hamsini wameokolewa.

Mmoja wa ndugu wa wahamiaji hao waliokuwa ndani ya boti Hassan Suleiman Daoud, amezitupia lawama, mamlaka nchini Misri kwamba zilikuwa zikishughulikia tatizo hilo taraatibu.
''...Tuliziambia mamlaka husika tangu majira ya saa kumi na moja na nusu kwamba boti inazama, lakini walikuwa wakisema hakuna boto ya uokoaji, na hakuna aliyekuwa akishughulikia...'' alisema Hassan.
Amefahamisha pia kwamba boti zao za uvuvi ndizo zilikuwa zikifanya kazi ya kuitafuta boti hiyo na kuokota maiti baharini na watoto pia kutoka ndani ya maji.
Amefahamisha pia kwamba wafanyabiashara haramu ya wahamiaji, wanatambuliwa na polisi katika maeneo haya pia amelaumu kuwa huchukua malipo ya mwezi kutoka kwao.
Katika kipindi cha mwaka huu pekee, wahamiaji wapatao laki tatu wamekatisha bahari ya Mediteranea na kuingia barani Ulaya, lakini njia yao kubwa ni ile ya kutokea Libya.