Jaji mmoja nchini Brazil amekubali mashataka ya rushwa dhidi ya Rais wa zamani wa nchi hiyo Luiz Ignacio Lula da Silva.
Atashtakiwa kwa madai ya kukubali kupokea zaidi ya dola za Kimarekani milioni moja wakati wa mradi mkubwa uliokuwa ukinuka rushwa katika kampuni ya mafuta ya serikali ya Petrobras.

Fedha hizo zinadaiwa kuhamishwa kupitia ununuzi wa ghorofa iliyokuwav ufukweni mwa bahari.
Hata hivyo, Lula da Silva mara nyingi amekuwa akikana madai hayo na kuyaita ni ya msukumo wa kisiasa.
Akiwa mmoja ya wanasiasa mashuhuri nchini Brazil, anatarajiwa kuwania tena nafasi ya urais katika uchaguzi katika kipindi cha miaka miwili.
Awali Lula da Silva alimchagua Dilma Rousseff, ambaye alivuliwa madaraka mwezi uliopita, kuwa ndiye mrithi wake