Vikosi maalum vya umoja wa mataifa nchini Syria vimesema vimeridhishwa na kupungua kwa mapigano tangu usitishwaji wa mapigano kuanza siku ya jumatatu.
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa Staffan De Mistura amesema kuwa anatarajia usambazaji wa misaada kuanza hivi karibuni,

Vikosi maalum huko Syria vimesema kuwa kuna utulivu maeneo mengi ya nchi
Image captionVikosi maalum huko Syria vimesema kuwa kuna utulivu maeneo mengi ya nchi

Amesema pia kipaumbele cha sasa ni kuandaa usambazaji wa misaada katika maeneo yaliyoshikiliwa na waasi huko Aleppo.
Mistura ameonya kuwa usitishwaji wa mapigano unaweza kuhatarishwa na athari za matukio ya vurugu yanayohusisha pande zenye mzozo.

Kwa mara ya kwanza imeripotiwa kutokuwepo kwa mauaji ya raia
Image captionKwa mara ya kwanza imeripotiwa kutokuwepo kwa mauaji ya raia

Wizara ya mambo ya nje ya Syria imeonya kuwa vifaa havitaruhusiwa kuingia Aleppo bila ruhusa yake.
Kusitishwa kwa mapigano kumeleta utulivu katika maeneo ya wakazi yanayoshikiliwa na waasi mjini Aleppo huku watoto wakicheza nje kwa mara ya kwanza bila kuwepo kwa ndege za mashambulizi, lakini Urusi imeshutumu waasi kwa ukiukaji zaidi ya mara ishirini nchi nzima wa makubaliano ya kusitisha mapigano na kuitaka Marekani kuweka nguvu kwa kundi wanalounga mkono.