Taifa la Tanzania ndilo lenye watoto wenye afya nzuri ya maungo duniani, kulingana na utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Australia.
Viwango vya afya ya maungo ya watoto milioni 1.1 walio kati ya umri wa miaka tisa hadi 17 kutoka mataifa 50 vilifanyiwa ukaguzi.

Watoto hao walifanyiwa zoezi la kukimbia umbali wa mita 20,ambalo hukagua afya yao ya maungo.
Grant Tomkinson, mmoja ya watafiti wakuu wa chuo cha Kusini mwa Australia ameiambia BBC kwamba watoto wa Tanzania waliibuka washindi kutokana na utendaji wao.