MWANAMITINDO ambaye pia ni muuza nyago kwenye video za Kibongo, Lulu Auggen ‘Amber Lulu’ ameweka wazi juu ya picha anazoposti kwenye mitandao ya kijamii zinazomuonesha akiwa nusu utupu kuwa haweki hivyo kutamanisha wanaume.

Akizungumza na Global TV Online kupitia kipindi cha Exclusive Interview mchana wa leo, Amber ambaye ametokea kwenye video kibao za Kibongo ikiwemo Too Much ya Darassa na Inde ya Dully alisema, wapo watu wengi wamekuwa wakimtumia meseji kwa kumtamani kisa wameona picha zake.

“Mi naposti kwa ajili ya biashara za nguo, navalishwa na kampuni then ninapoposti nguo ile inakuwa sokoni sasa kuna watu wengine wanakuja juu kwa kunitamani sa nawashangaa huko kunitamani vipi?,” alisema Amber.
Amber pia alizungumza juu ya mastaa aliotoka nao kimapenzi hadi sasa na kusema kuwa wanazidi 100.