Baadaye atafanya ziara fupi kwenye Kampuni ya kusafirisha mizigo inayomilikiwa na Serikali ya Zambia inayojulikana kama Zamcargo, kisha ataelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) ambako ataagwa rasmi na mwenyeji wake Rais Magufuli kurejea nchini kwake Zambia.
Katika taarifa hiyo ya Mambo ya Nje inaeleza kuwa ziara ya Rais Lungu inatarajiwa kutoa fursa ya kuzidisha uhusiano na kukuza ushirikiano ili kuongeza ufanisi wa Reli ya Tazara ambayo ni mhimili na kiungo muhimu katika ukuzaji wa uchumi wa Tanzania na Zambia, lakini pia na kwa nchi nyingine majirani za ukanda wa kusini na kati mwa Afrika za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Zimbabwe na Malawi.
Pia eneo lingine litakuwa ni kukuza ushirikiano katika matumizi ya bomba la Tazama ambalo lilijengwa mwaka 1968 kwa lengo la kutoa njia nafuu ya kusafirisha mafuta ghafi kwenda nchini Zambia na hivyo kuiepusha nchi hiyo na athari za kupanda kwa bei ya mafuta. Hata sasa umuhimu wa bomba hilo bado upo.
Eneo lingine litakuwa ni ushirikiano katika matumizi ya Bandari ya Dar es Salaam ambayo kwa muda mrefu Zambia kama nchi ambayo haina bandari imekuwa ikitumia Bandari ya Dar es Salaam kupitisha mizigo yake. Kwa sababu za kiuchumi na za kihistoria, nchi hiyo imeendelea kuwa mdau mkubwa katika matumizi ya bandari hiyo.
Rais Deby
Taarifa iliyotolewa na serikali inaonesha Rais Deby ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na watapata fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Ukanda wa Afrika Mashariki na Umoja wa Afrika kwa ujumla.
Deby amefuatana na mkewe, Hinda Deby, Moussa Faki Mahamat ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje, Mtangamano wa Afrika, na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chad na viongozi wengine waandamizi wa Serikali ya Chad.
|
0 Comments