Meya huyo aliandika chini ya ujumbe huo wa kibaguzi, “Just made my day Pam.”
Zaidi ya watu 200,000 wamejiandikisha mtandaoni ndani ya muda mfupi kupinga ubaguzi huo na kuwataka Whaling na Taylor kujiwajibisha haraka.
Vitendo vya kibaguzi vimeripotiwa kuongezeka nchini humo tangu Trump alipotangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais.
Ingawa kauli zake wakati wa kampeni zilikuwa na matamko tata, Trump amewataka wafuasi wake kuacha mara moja vitendo vyovyote vya kibaguzi akisisitiza kuwa yeye atakuwa rais wa Wamarekani wote.
0 Comments