Zaidi ya wahitimu laki mbili nchini Nigeria ambao hawakuwa na ajira wameanza kupokea ujumbe mfupi unaowataarifu kuwa wameajiriwa na mchakato maalumu wa ajira wa serikali.

Wamekuwa ni awamu ya kwanza kupata ajira kati ya waliohitimu kufuatia ahadi ya kutoa ajira kwa zaidi ya wahitimu nusu millioni nchini Nigeria iliyotolewa na serikali katika uchaguzi mkuu mwaka uliopita.
Watakuwa wakilipwa karibia dola millioni mia moja kwa mwezi.
Ofisi ya waziri mkuu imeeleza kwamba zaidi ya wahitimu laki moja katika awamu ya kwanza ni walimu, na wengine laki tatu wataajiriwa katika sekta ya kilimo na watakaobakia watakuwa katika sekta ya Afya.