Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetoa taarifa kuwa kuanzia saa 9 alasiri
leo Januari 30, 2017 njia ya reli kati ya Kituo Kikuu cha Dar es salaam na Ruvu
imefunguliwa rasmi kwa shughuli za uendeshaji wa reli.
Taarifa hiyo imesema kuwa kazi ya ufunguaji njia imewezekana baada ya Wahandisi na
Mafundi wa reli kuyaondoa Mabehewa yaliopata ajali l kutoka relini na pia kuikarabati
sehemu iliyo haribika . Kazi hiyo imefanyika kuanzia usiku wa Januari 29, 2017 hadi
mchana wa Januari 30, 2017.
Aidha treni ya abiria iliyoahirisha safari ya kuondoka kwenda bara jana imeondoka leo
saa 9:05 alasiri kutoka kituo kikuu cha Dar es Salaam kwenda bara..
Wakati huo huo imefahamika kuwa msafiri mmoja aliyetambulikana kama Nd Basekena
O. Bango kutoka Bujumbura Burundi akiwa anasafiri kutoka Kigoma amelazwa katika
Hospitali ya Tumbi Kibaha mkoani wa Pwani kwa ajili ya matibabu zaidi. Aligunduliwa
kuwa amechanika mguu wake wa kulia hivyo basi kuhitaji kushonwa mguu wake huo.
Taarifa kutoka Muhimbili zinaeleza kulazwa kwa majeruhi wawili waliopokelewa
hospitalini hapo usiku wa Januari 29, 2017. Majeruhi wamefamika kuwa ni Nd.
Stephania Mbona (46) kutoka Kigoma alikuwa amekuja Muhimbili kuendelea na
matibabu ya ugonjwa wa tumbo, hata hivyo alitibiwa majeraha ya kawaida na
anaendelea kulazwa kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wake wa tumbo.
Mgonjwa wa pili Nd Alice Jovin (37) mkazi wa Salasala Dar es Salaam alikuwa anatoka
Kigoma kuja Dar es Salaam amepata majeraha ya kawadia ametibiwa na alitarajiwa
kuruhusiwa leo asubuhi.
Kuhusu idadi ya wasafiri treni ya Deluxe yenye uwezo wa kusafirisha abiria zaidi ya
1000 wakati inapata ajali ilikuwa na abiria 480.
Aidha imefahamika kuwa ili kufahamika hasara na sababu za ajali hiyo taarifa rasmi
itatolewa baada ya uchunguzi wa Kamati maalum inayoundwa kwa mujibu wa sheria,
taratibu na kanuni za uendeshaji reli za kimataifa. Taarifa hiyo itatolewa baada ya wiki
mbili.
Imetolewa na Afisi ya Uhusiano:
Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TRL
Ndugu Masanja Kungu Kadogosa
Januari 30, 2017
DAR ES SALAAM |
0 Comments