Angola imeripoti visa viwili vya kwanza vya ugonjwa wa Zika kwa mujibu wa shirika la Reuters.
"Hadi miezi miwili iliyopita, hatukuwa na kisa chochote, lakini sasa tuna visa viwili vya Zika," Reuters ilimnukuu waziri wa afya wa nchi hiyo José Luis Gomes Sambo.

Lazima tuchukue hatua za kuzuia, hasa katika kukabiliana mbu."
Zika ni ugonjwa unaosambazwa na mbu na umesembaa kwenda nchi kadha tangu uibuke nchini Brazil mwaka 2015.
Ugonjwa huo unaaminiwa kusababisha madhara kwa watota wanaozaliwa.