DC
KOROGWE AWAONYA WATUMISHI WA HALMASHAURI KUACHA KUTUMIA VIBAYA FEDHA
ZA MIRADI YA MAENDELEO.


Mkuu wa wilaya ya Korogwe
Mkoani Tanga,Mhandisi Robert Gabriel akizungumza jambo na Mkurugenzi
wa Taasisi ya
isiyoyakiserikali
ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha Azidu Kaonekana wa pili
kulia ambao wameshirikiana na A Better World kutoka Canada kufanya
ujenzi wa majengo matatu ya maabara kwenye shule ya sekondari ya Patema
iliyopo kata ya Mpale Wilayan

Kaimu Afisa Elimu Sekondari
Halmashauri ya Korogwe Vijijini,Martha Kusare kulia akipokea msaada wa
sola ya mobisol  kutoka kwa Mkurugenzi wa Taasisi isiyoyakiserikali ya
Vuga Development
Initiative ya
Jijini Arusha,Azidu Kaoneka ikishirikiana na A Better World kutoka
Canada kwa shule ya sekondari ya Patema ili kuweza kutumia nishati ya
umeme kwa ajili ya matumizi yao ambapo sola hiyo na
ujenzi wa maabara tatu zilizojengwa na
taasisi hiyo  iligharimu kiasi cha sh.milioni
75
Mkurugenzi
wa Taasisi isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini
Arusha,Azidu Kaoneka akifuatilia maendeleo ya wanafunzi wa shule ya
sekondari Patema wilayani korogwe Mkoani Tanga
Mkurugenzi wa Taasisi
isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu
Kaoneka kulia akiteta jambo na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Patema
Jerome Massawe wakati wakitembelea maabara hiyo
Mkurugenzi wa Taasisi
isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu
Kaoneka wa pili kulia akiangalia namna wanafunzi wa shule ya sekondari
Patema wanayofundishwa masomo ya sayansi mara baada ya kukamilika
maabara hiyo
Mkurugenzi wa Taasisi
isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha,Azidu
Kaoneka kulia akiteta jambo na mwalimu mkuu wa shule ya sekondari
Patema,Jerome Massawe
 Muonekano wa Majengo
ya  maabara hizo




WATUMISHI katika Halmashauri ya
wilaya ya Korogwe mkoani Tanga wameonywa kuacha kutumia vibaya fedha za
miradi zinazotokana na wafadhili kwenye maeneo yao kwani watakaobainika
kufanya hivyo watashughulikiwa ikiwemo kufikishwa kwenye vyombo vya
sheria.


Hayo yalisemwa  na Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mhandisi Robert

Gabriel wakati akipokea taarifa ya
umalizaji wa majengo ya matatu ya maabara yalijengwa na taasisi
isiyoyakiserikali ya Vuga Development Initiative ya Jijini Arusha
ikishirikiana na A Better World kutoka Canada kwa shule ya sekondari ya
Patema iliyopo kata ya Mpale Wilayani humo.


Aidha wao kama viongozi wa serikali wilayani humo hawatakuwa na
mdhara

na watumishi ambao watabainika kuihujumu
miradi ya maendeleo inayopelekwa kwenye maeneo yao na wafadhili
mbalimbali kwani kufanya hivyo kunachangia kurudisha nyuma kasi ya
ukuaji wa maendeleo.


“Nisema wazi kuwa watumishi badilikeni kwani mimi kama kiongozi wa

wilaya hii sitamfumbia macho mtu yeyote
ambaye atakuwa kikwazo cha maendeleo kwenye wilaya hii na niwaonye wenye
tabia kama hiyo waiache mara moja.


Aidha alisema lazima watu wabadilike hasa wale wanaopewa majukumu
ya

kusimamia miradi hiyo kutoka kwa
wafadhili na wawe wawazi wakati wa utekelezaji wake ili kujenga heshima
kwa jamii na Taifa kwa ujumla.


“Baadhi yetu tunatumia fursa hizo vibaya na kujinufaisha kupitia
fedha

za wafadhili kinyume na hitaji
husika,kufanya hivyo kunaweza kuwakimbiza wadau hao wa maendeleo na
kutia doa kwa Taifa”Alisema Gabriel.


Awali akizungumza katika kikao hicho Afisa Elimu sekondari
Halmashauri

ya Korogwe Vijijini Patricia Mbigili
alisema pamoja na jitihada kubwa ambazo wanazifanya kuhakikisha
wanakamilisha suala la maabara lakini mpaka sasa zilizokamilika ni 5
kati ya 78 katika shule 26,ambapo kunahitajika maabara 3 kwa kila shule
ikiwa ni za chemia,physician na bioligia.


Alisema ili kukabiliana na tatizo la ufaulu wa masomo ya sayansi



katika shule za sekondari maabara na uwepo wa walimu wa masomo hayo
unahitajika kwa kiasi kikubwa ili kuweza kuwajengea uwezo wanafunzi
kujifunza kwa vitendo.


Mbigili alisema jukumu la kuboresha miundombinu ya shule na makazi
ya

walimu ni la wananchi wote,serkali na
taasisi zinazojitolea ili kutimiza azma ya serikali ya kuboresha sekta
ya elimu kama ilivyoanza kwa madawati na elimu bure.


Naye kwa upende wake, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Azidu Kaoneka

alisema umaliziaji wa maabara 3,nyumba 1
ya walimu na kuwawekea kifaa cha kuzalisha umemekupitia jua (mobisol)
ambapo kiasi cha shilingi milioni 75 zimetumika.


Azidu alisema taasisi hiyo inaimani kubwa kwa kushirikiana na wananchi

pamoja na serikali wanaweza kujenga
mazingira rafiki ya walimu na wanafunzi kwa kuboresha miundombinu ya
mashule pamoja na nyumba za walimu kama ilivyofanyika shuleni
hapo.

Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.