Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa TANZANIA Dkt. John Pombe Magufuli ametoa wito kwa Mahakama kukusanya
Shilingi Trillioni 7.3 ambazo ni matokeo ya serikali kushinda kesi mbalimbali za
ukwepaji kodi.





Rais Magufuli ameyasema
hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya siku ya Sheria na Mwaka
mpya wa Mahakama iliyobeba kauli Mbiu isemayo Utoaji haki kwa wakati kuwezesha
ukuaji wa uchumi.





Alisema  kuwa Takwimu zinaonesha kuwa kumekuwa na baadhi
ya kesi za pingamizi za kodi ambapo  Serikali imeshinda kesi hizo japo  fedha hizo hazijakusanywa mpaka sasa.“Kukwepa au kutolipa
kodi ni kosa kubwa sana, kila mtu anawajibu wa kulipa kodi nchini kwa maendeleo
ya nchi” nalifafanua Dkt Magufuli.


Aidha, Rais Magufuli
alisema kuwa katika kuelekea ukuaji wa uchumi, Mahakama iwe sehemu ya chanzo
cha pato la taifa kwa kwa kuhakikisha wale wanaotakiwa kulipa fidia baada ya
kushindwa kesi wanafanya hivyo pamoja na kuwabana wakwepa kodi kwani kutimiza
hilo kutaleta mabadiliko katika uchumi wa nchi.
Na Beatrice
Lyimo - MAELEZO.