Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa akiwasili katika msikiti wa Riadha mjini Moshi kwa ajili ya Swala ya Eid el Fitri iliyofanyika kitaifa mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa katika Msikiti wa Riadha mjini Moshi.

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa aikishiriki Swala ya Idd el Fitri iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu wakishitiki Swala Idd.
Swala ya Idd ikifanyika katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Tanzania,Kassim Majaliwa,akiwa na Sheakh Mkuu wa Tanzania ,Mufti Abubakary Zubery ,Waziri wa Maliasili na Utalii,Prof Jumanne Maghembe pamoja na Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu ,Said Mwema.
Mshindi wa kuhifadhi Quran tukufu ,Ibrahim Mitigo akionesha namna ambavyo alivyohifadhi Quran wakati wa Swala ya Idd el Fitry iliyofanyika katika msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki Swala ya Idd mjini Moshi.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ,akizungumza wakati wa Swala ya Idd el Fitry iliyofanyika kitaifa katika Msikiti wa Riadha mjini Moshi.
Mufti wa Tanzania na Sheakh Mkuu,Abubakary Bin Zubery akitoa nasaha zake wakati wa Swala ya Idd iliyofanyika kitaifa mjini Moshi.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakishiriki katika Swala ya Idd El Fitry iliyofanyika mskiti wa Riadha mjini Moshi

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini.

SERIKALI
imeahidi kuongeza kasi katika zoezi la ukamataji wa wahusika wa matukio ya
mauaji yaliyotokea Kibiti,Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani na kuhakiksha
wanafikishwa mbele ya vyombo vya sharia.
Waziri
Mkuu wa Tanzania ,Kassim Majaliwa aliyasema hayo jana katika baraza la Idd
lililofanyika kitaifa katika mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro lkitanguliwa na
Swala ya Idd El Fitri iliyofanyika kitaifa katika msikiti wa Riadha.
“Kinachofanyika
sasa nikuhakikisha kwanza tunawapata waharifu halisi ilikuepuka kuingiza watu
wasio husika, kama vile hao wenye hisia kwamba mauaji haya yanafanywa labda na
waislamu hapana .”alisema Mh Majaliwa .
Alisemakaz
kubwa inayofanywa sasa ni kuchuja na kujua nani hasa anshiriki katika mauaji
hayo huku akiwashukuru watanzania ambao tayari wameanza kutoa ushirikiano kwa
kuanza kueleza nani wanahusika katika tukio hilo.
“Kazi
yetu ni kuwapeleleza pale ambapo tunauthibitisho wa ushiriki wao na hatua kali
zitachukuliwa dhidi yao na kazi hiyo inaendelea vizuri.”alisema Majaliwa.
Mapema
katika taarifa ya Baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) iliyosomwa na kaimu
katibu Mkuu,Sheakh Salim Amir Abeid alisema Bakwata imeshtushwa na matukio ya
mauaji ya kutisha ya watu wasio na hatia katika maeneo ya mkoa wa Pwani.
Alisema
kutokana na matukio hayo Baraza kuu linatoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu
na jamaa zao katika matukio hayo aliyoyataja kutokuwa na hata chembe ya
kibinadamu .
“Kumekuwepo
na matukio ya kutisha ya mauaji ya watu wasio na hatia katika maeneo ya mkoa wa
Pwani,matukio ambayo yametushtua sana na kuisikitisha mioyo yetu,baraza kuu la
waislamu la Tanzania kwanza kabisa linatoa pole kwa familia zilizopoteza ndugu
na jamaa zao katika matukio hayo ya kinyama yasio na chembe ya kibinadamu hata
kidogo.”alisema Abeid
Alisema
Bakwata inasikitishwa na vitendo vyenye viashiria vya kutaka kuichafua dhima
nzuri ya Tanzania kuwa ni kisiwa cha amani na utulivu hasa pale matukio hayo
yanapo husishwa na na Dini ya Kiislamu.
“Uislamu
ni dini ya amani upendo kuvumilia na nakuishi pamoja na watu wa imani tofauti
na kwamba yeyote afanyae matendo yoyote na kinyama kama hayo katu haiwakilishi
uislamu na baraza linawataka waislamu kushikamana.”alisema Abeid.

Mwisho.