Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na vilabu vya Psg, Barcelona na Ac Milan Ronaldo de Assis Moreira Maarufu kama Ronadinho Gaucho amestaafu soka.
Licha ya Ronadinho kutocheza soka la kiushindani toka mwaka 2015 amekua akicheza michezo ya mabonanza

Kaka na wakala wa mchezaji huyo Roberto Assis amethibitisha kuwa umefika mwisho kwa fundi huyo wa kibrazil kucheza soka.
Ronaldinho alianzia soka lake katika klabu ya Gremio ya nchini kwao kabla ya kujiunga na Paris St-Germain mwaka 2001 na baadae kujiunga na Barcelona alikongara sana.
Katika msimu wa 2010 -2011 alijiunga na Ac Milan ya Italia kabla ya kurudi kwao na kujiunga na Flamengo mwaka 2011. Kisha alichezea vilabu vya Atletico Mineiro, na Queretaro ya nchini Mexico na kurudi tena kwao Brazil katika klabu ya Fluminense.