Katibu mkuu wa Enzi Foundation na mbunifu wa mavazi wa Holland Fashion Bi.Bahia Kihondo akifungua rasmi Usiku wa Mtanzania hapo jana katika jiji la Den Haag nchini Uholanzi.Kulia ni Muhasisi Muandamizi na Mwenyekiti wa Enzi Foundation Bi Rehema Simkoko.

Mwenyekiti wa Enzi Foundation Bi Rehema Simkoko akielezea historia fupi na malengo ya taasisi yake kwa wageni waalikwa waliohudhuria ukumbini hapo jana katika jiji la Den Haag nchini Uholanzi.


Mwenyekiti wa Enzi Foundation Bi.Rehema Simkoko akitoa tuzo kwa Mwenyekiti wa Stuchting Africa Life nchini Uholanzi,Enzi Foundation imemtunuku tuzo hiyo kwa mchango wake mkubwa ndani ya Enzi Foundation. 

Mwenyekiti wa Enzi Foundation Bi.Rehema Simkoko akimtunuku tuzo ya kumuenzi Mzee Hamidu, mmoja wa wazee wenye Upendo na waendelezaje bora wa Mila na tamaduni zetu nje ya nchi.

Usiku wa Mtanzania ulikuwa bora kwa Maganga One Blogger baada ya kutunukiwa tuzo ya mwanahabari bora barani Ulaya,Maganga One alitunukiwa Tuzo hiyo kutoka kwa Uongozi mzima wa Enzi Foundation sherehe za usiku wa Mtanzania zilifanyika jijini Den Haag nchini Uholanzi.

Mwanamuziki kutoka nchini Angola anakwenda ka jina Alzira Assis akitumbuiza kwenye usiku wa Mtanzania huku wageni waalikwa wakiwa makini kumsikiliza jinsi anavyoburudisha

Wanamitindo ambao waliupamba usiku wa Mtanzania hapo jana katika jiji la Den Haag wakipita mbele ya jukwaa kuwaonyesha wageni mbalimbali mavazi yaliyobuniwa na Holland Fashion chini ya mbunifu Bahia Kihondo

Wageni waalikwa kutoka nchini mbalimbali wakifuatilia usiku wa Mtanzania hapo jana

Mmoja wa wanamitindo akipita mbele ya wageni waalikwa kwenye usiku wa Mtanzania na vazi la kitenge lililobuniwa na mwanadada Bahia Kihondo wa Holland Fashion.

Kiukweli Usiku wa Mtanzania ulipendeza kwa mavazi mbalimbali yaliyobuniwa na Holland Fashion

Wageni waalikwa wakipiga makofi kuupongeza uongozi wa Enzi Foundation

Wageni waalikwa wakifuatilia mambo yanayojiri usiku wa Mtanzania ulioandaliwa na Enzi Foundation

Usiku wa Mtanzania ulipendeza kihivii...Full vitenge mpaka raha Gebo Family

Wageni kutoka Ubelgiji ambao nao walihudhuria usiku wa Mtanzania nchini Uholanzi

Burudani ya mziki ikitumbuizwa na mwanadada kutoka nchini Angalo kwa jina la Alzira Assis huku wanamitindo wakipita na mavazi ya Kanga.


Katibu mkuu wa Enzi Foundation na Mbunifu wa mavazi wa Holland Fashion Bi.Bahia Kihondo akipita kwa utambulisho huku akipigiwa makofi na wanamitindo wake{Picha zote na maelezo kutoka Maganga One Blog}

Burudani ya muziki ilichukua nafasi na watu wakaselebuka

Dj Andrew wa nchini Uholanzi akiwa na Dj Jamal kutoka Ubelgiji wakia kazini kuhakikisha 

Mrembo wa miaka yote mwanamama Sexy mama katika ubora wake ndani ya usiku wa Mtanzania

Huku burudani zikiendelea watu walikuwa makini kuhakikisha hawapitwi na kila kinachoendelea jukwaani ndani ya usiku wa Mtanzania.


Usiku wa Mtanzania na mavazi ya kitanzania,hapa wageni waalikwa wakifurahia baadhi ya mambo ukumbuni

Vazi la kanga likitawala jukwaa

Moja ya ubunifu wa Holland Fashion 

Wanamitindo wakiwa jukwaani kuonyesha mavazi yaliyobuniwa na mwanamitindo Bahia Kihondo wa Holland Fashion.{Picha zote na Maganga One Blog}


Mwanamuziki Alzira kutoka Angola akiendelea kutumbuiza katika usiku a Mtanzania nchini Uholanzi

Vazi la kanga likichukua nafasi yake

Wanamitindo wakiwa katika vazi la kanga 

Hapo ndipo wakati wa kuonyeshwa vitu asilia ambavyo mpaka leo vinatumika kwa matumizi ya jikoni kwa sisi waafrika,nani ambae haujui Ungo,ukizungumzia Chungu nacho hakuna mtu hasiyevifahamu vitu hivyo.

Mavazi ya asili ya Kimasai nayo yalileta raha yake katika kuyaangalia jukwaani

Mc wa jana alikuwa ni ndugu Abeka kutoka Radio Africa Europe ambaye aliupamba vyema usiku wa Mtanzania 

Kitenge au kanga ubunifu huu wote utaupata kutoka Holland Fashion chini ya mbunifu wa mavazi B.Bahia Kihondo ambaye anapatikana kwa njia ya isntagram @hollandfashion

Mwenyekiti na muhasisi wa Enzi Foundation Bi.Rehema Simkoko akisakata nyimbo za kale ndani ya usiku wa Mtanzania


Kijana mdogo ambaye alikuwa akishangiliwa kila anapopita jukwaani kwa jinsi alivyokuwa anapendeza na mavazi yote aliyopita nayo

DUMISHENI UPENDO,AMANI,UTULIVU NA UMOJA ni moja kati ya maneno ambayo yataenziwa siku zote na baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.