ILIKUWA patashika nguo kuchanika katika Uwanja wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara kwenye tamasha la Wasafi Festival usiku wa Novemba 24, ambapo wasanii kutoka WCB wakiongozwa na Diamond Platnumz, wameangusha bonge moja la shoo ya kukata na shoka.


Miongoni mwa mastaa waliohudhuria ni pamoja na waigizaji kutoka Bongo Muvi, ambapo Jacquline Wolper, alipopata nafasi ya kuwasalimia wana Mtwara shangwe likalipuka kwa wakazi hao kumuita shemeji na kelele zilivyonoga akatangaza kuwa anarudiana rasmi na mpenzi wake wa zamani Harmonize.