Waziri Yoav Gallant

Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant amemtaka Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kufanya mazungumzo ya kusitisha mapigano na Hamas ili kuwarudisha nyumbani mateka waliosalia kutoka Gaza.

Katika taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa X uliojulikana kama Twitter zamani, Gallant amesema "Muda umeisha kwa watu waliotekwa na kuawa bila hatia yoyote.”

"Lazima mateka ambao bado wanashikiliwa na kundi la Hamas warudishwe nyumbani."

Ombi lake linakuja baada ya miili sita ya mateka kupatikana katika handaki la chini ya ardhi huko Rafah kusini mwa Gaza.