Mahakama ya juu zaidi nchini Afrika Kusini imeamua kuwa wanaume wanaweza kutumia jina la ukoo la wake zao, na kubatilisha sheria iliyowazuia kufanya hivyo.
Katika ushindi wa wanandoa wawili walioleta kesi hiyo, Mahakama ya Kikatiba iliamua kwamba sheria hiyo ilikuwa "ungiaji wa kikoloni" ambao ulilingana na ubaguzi wa kijinsia.
Henry van der Merwe alinyimwa haki ya kutumia jina la ukoo la mke wake Jana Jordaan, wakati Andreas Nicolas Bornman hakuweza kujumuisha Donnelly, jina la ukoo la mkewe, Jess Donnelly-Bornman, kituo cha habari cha SABC, kinaripoti.
Bunge sasa litalazimika kurekebisha Sheria ya Usajili wa Vizazi na Vifo, pamoja na kanuni zake, ili uamuzi huo uanze kutekelezwa.

0 Comments