Mapigano yamepamba moto mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo siku ya Ijumaa, siku moja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kuwakaribisha viongozi wa Congo na Rwanda mjini Washington kutia saini mikataba mipya inayolenga kumaliza mzozo wa miaka mingi katika eneo lenye utajiri mkubwa wa madini.
Rais wa Congo Felix Tshisekedi na Paul Kagame wa Rwanda siku ya Alhamisi walithibitisha ahadi zao kwa makubaliano yaliyofikiwa mwezi Juni ili kuleta utulivu katika nchi hiyo na kufungua njia kwa uwekezaji zaidi wa madini wa Magharibi.
"Tunasuluhisha vita ambavyo vimekuwa vikiendelea kwa miongo kadhaa," alisema Trump, ambaye utawala wake umeingilia kati msururu wa vita duniani kote.
Hata hivyo, mapigano makali yaliendelea huku pande zinazopigana zikilaumiana.
Kundi la waasi la AFC/M23 linaloungwa mkono na Rwanda, liliteka miji miwili mikubwa mashariki mwa Congo mapema mwaka huu na halifungamani na makubaliano ya Washington, lilisema vikosi vinavyoitii serikali vinaendesha mashambulizi mengi.
Kwa upande wake, msemaji wa jeshi la Congo amesema mapigano yanaendelea.

0 Comments