Idara ya Usalama ya Marekani inachunguza milio ya risasi iliyosikika karibu na Ikulu ya White House mapema Jumapili asubuhi.
Maafisa walijibu ripoti za milio ya risasi katika eneo linalozunguka Hifadhi ya Lafayette ya Washington DC muda mfupi baada ya saa sita usiku kwa saa za eneo (04:00 GMT) na kushika doria katika bustani hiyo, kaskazini mwa makazi ya rais, na eneo linalozunguka, Idara hiyo ilisema.
Kulingana na Idara ya Usalama hakuna mshukiwa aliyepatikana na hakuna majeraha yaliyoripotiwa. Idara hiyo na washirika wake wanatafuta gari linalowezekana kuhusishwa na tukio hilo na mtu anayehusika.
Rais Donald Trump alikuwa Washington DC wikendi hii. Idara ya Usalama ilisema shughuli katika Ikulu ya White House zinaendelea kama kawaida lakini "usalama umeimarishwa".
Uchunguzi ulifunga baadhi ya barabara katika eneo hilo, lakini zimefunguliwa tena, msemaji wa Jeshi la Polisi Anthony Guglielmi alisema katika ujumbe kwenye mtandao wa X.
Mwakilishi wa Idara ya Upelelezi aliithibitishia BBC Jumapili jioni kwamba "uchunguzi unaendelea".
Katika ujumbe kwenye mtandao wa X, mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu ya White House, Steven Cheung, alisema siku ya Jumamosi kwamba Trump "amekuwa akifanya kazi mfululizo katika Ikulu ya White House" wikendi hii ya Pasaka.

0 Comments