BBC Verify imekuwa ikifuatilia meli ambazo zinapita katika mlango bahari wa Hormuz, baada ya idara inayosimamia jeshi la Marekani Centcom, kutangaza kuwa wataifunga mlango huo wa bahari na kuzuia meli zote zinazoingia na kutoka bandari ya Iran.
Tangu Centcom kutoa taarifa hiyo usiku wa jana, meli nne zimeonekana zikipita mlango huo wa bahari kulingana na data iliyotolewa na shirika la ufuatiliaji la MarineTraffic.
Meli hizo, zote nne ni za kubeba mafuta au gesi,ila hazijatambuliwa kama zinamilikiwa na Iran, au zinatoka au kuingia katika bandari ya Iran.
Centcom imetangaza kuwa manowari mawili USS Frank Peterson Jr na USS Michael Murphy, ziko karibu na eneo hilo na zitatumika kuondoa mabomu ya bahari yaliyokuwa yameekwa na jeshi la Revolutionary Guard la Iran.
BBC Verify, inaendelea kufuatilia meli zinazopita katika mlango huo wa bahari huku makataa ya Marekani yakikaribia kutamatika.

0 Comments