Mwanamfalme Harry

Duke wa Sussex Mwanamfalme Harry na watu wengine sita wameshindwa kesi yao kuhusu faragha katika Mahakama Kuu dhidi ya kampuni inayochapisha magazeti ya Daily Mail na Mail on Sunday

Kundi hilo, ambalo linajumuisha Sir Elton John, Baroness Lawrence na Liz Hurley, liliishtaki kampuni ya Associated Newspapers Limited (ANL) kwa madai ya kukusanya taarifa kinyume cha sheria.

Katika uamuzi wake, Jaji Nicklin amesema madai hayo ni mazito na yanahitaji ushahidi zaidi wa kushawishi kabla ya kuthibitishwa - lakini walalamikaji walishindwa kuyathibitisha.

Kesi ya wiki moja ilishuhudia Mwanamfalme Harry akitoa ushahidi kuhusu makala alizozilalamikia akisema kampuni hiyo imefanya maisha ya mkewe kuwa "maumivu makubwa."

Akijibu uamuzi huo, ANL ambayo inachapisha magazeti hayo imesema ni "uthibitisho wa uandishi wa habari wa Daily Mail."