Wana watatu wa aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei, Maysam, Massoud na Mustafa Khamenei, walionekana katika mstari wa mbele wakati wa sala ya mazishi ya baba yao katika msikiti mmoja mjini Tehran.

Hata hivyo, kwa mujibu wa BBC Persian, mwanawe wa nne, Mojtaba Khamenei, ambaye ni Kiongozi Mkuu wa sasa wa Iran, hakuhudhuria sala hiyo.

Kwa mujibu wa Reuters Mojtaba Khamenei ambaye sasa anaiongoza Iran amezuiwa kuhudhuria mazishi ya baba yake kwa sababu za kiusalama.

Ali Khamenei aliuawa mapema mwaka huu katika shambulizi la ndege isiyo na rubani lililotekelezwa na Marekani na Israel.

Sala za mazishi ziliongozwa na Ayatollah Jafar Sobhani katika Msikiti wa Imam Khomeini, moja ya vituo vikuu vya kidini na kitamaduni mjini Tehran.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA, sala hizo zilifanyika katika hatua tatu. Hatua ya kwanza ilihusisha sala ya mazishi ya Ali Khamenei. Hatua ya pili ilihusisha sala za mazishi za binti yake Bushra Khamenei, mkwe wake Misbah al Huda Baqeri, na shemeji yake Zahra Haddad Adel.

Hatua ya tatu ilihusisha sala ya mazishi ya mjukuu wake mdogo, Zahra Mohammadi