Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa Mlango bahari wa Hormuz ni eneo la Marekani.

“Kwa sasa natangaza Mlango wa Hormuz kuwa eneo la Marekani.”

Akifanya kampeni katika jimbo la South Carolina, Trump alisisitiza kuwa hawataruhusu Iran kumiliki silaha za nyuklia.

Kauli hizo mpya zinakuja wakati Marekani imeongeza shinikizo la kiuchumi dhidi ya Iran katika siku za hivi karibuni, huku ikiendelea kuweka kizuizi cha kijeshi katika eneo hilo la bahari.

Washington inatarajiwa kutangaza siku ya Jumatatu vikwazo vipya dhidi ya Iran. Maafisa wa Marekani wanasema vikwazo hivyo vinaweza pia kuathiri washirika wakuu wa kibiashara wa Iran, ikiwemo China.