Takriban watu 22 wamefariki katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Kinshasa, baada ya moto kuzuka kwenye sherehe ya harusi.
Kwa mujibu wa mamlaka nchini humo, moto huo ulitokea jana usiku na kuendelea kwa saa kadhaa. Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.
Meya wa Lingwala, Norbert Mushinga, amesema idadi ya waliofariki inaweza kuongezeka kwa kuwa watu wengi walikuwa wakishiriki katika sherehe hiyo.
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani wa DRC, Jacquemin Shabani, alitembelea eneo la tukio na kulielezea kuwa ni "janga".
Tukio hilo ni la hivi karibuni katika mfululizo wa moto iliyosababisha vifo Kinshasa, hasa katika maeneo yenye watu wengi ambako huduma za kuzima moto na miundombinu ya mijini ni hafifu.
0 Comments