Serikali yenye utata ya Rais Laurent Gbagbo imepiga marufuku ndege za majeshi ya usalama ya Umoja wa Mataifa na Ufaransa kupita kwenye anga ya nchi hiyo, au kutua Ivory Coast.
Tamko hilo limetolewa huku Alassane Ouattara, anayetambulika na Umoja wa Mataifa kama mshindi wa uchaguzi uliofanyika mwezi Novemba, alipokwenda kwenye mkutano nchini Ethiopia juu ya mgogoro huo.