Mwakilishi wa kituo cha watoto yatima cha Mwandaliwa, Haji Bakula (kulia) akipokea mfuko wa sukari kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Twiga Cement, Pascal Lesoinne (katikati) kwenye ofisi za Mfuko wa Maendeleo na Wanawake (WAMA) jijini Dar es Salaam. Vituo vitatu vya watoto yatima vilipata misaada ya vyakula vyenye thamani ya shilingi milioni 15 kutoka kwa kampuni hiyo. Wanaomsaidia kukabidhi ni Kaimu Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Jordan Rugimbana (wa pili kushoto), Katibu Mtendaji wa WAMA, Daudi Nasib (kushoto) na Ofisa Uhusiano na Huduma kwa Jamii wa Twiga Cement, Natasha D’Souza. (Picha na Robert Okanda).